Kuzaliwa upya
- Mhubiri,mmoja akipokea akiendesha magufuri kule Moscow, urusi Mnamo mwezi machi,1992,alivamiwa ofisini na kijana mmoja mwenye nguvu na sura ya kutisha. Mhubiri yule aliogopa, lakini baada ya muda mkalimani wake alimjulisha Kuwa yule kijana alikuwa ni mmoja wahalifu walioshindikana Moscow. Alikuwa amefungwa jela Mara nyingi.sasa alikuwa akijisikia hatia na hakuwa na amani.Mhubiri yule alimsomea 1 yoh.1:9,"Tukiziungama dhambi zetu, yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu na kutusafisha na udhalimu wote "
Alimsimulia kisa cha yule Mwizi msalabani aliyesamehewa na yesu akiwa juu ya msalaba.Alimhakikishia Kuwa yesu bado anaokoa hata sasa.Anasamehe.Mhubiri alimtia moyo yule kijana ampokee Yesu. Yule kijana kijana,huku akitokwa na machozi, alipiga magoti na kupokea msamaha wa Yesu.
Baada ya mwaka mmoja, Mhubiri yule alitembelea tena Moscow na kumwona yule kijana akimsifu Mungu katika Kwaya.baada ya kumpokea Yesu, alikuwa amebadilika na kubatizwa.
Ubatizo ni ishara ya kuanza maisha mapya. Ni kuzaliwa upya.
Je, Ubatizo ni wa lazima?
"aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini,atahukumiwa. " Mk.16:16
Jambo hili liko wazi. Ubatizo ni moja kati ya mahitaji kwa ajili ya wokovu
- Siku hizi kuna Ubatizo wa Aina nyingi. Je, wowote Kati ya huo si unakubalika mradi anayebatizwa awe mwaminifu?
"Bwana mmoja, imani moja, Ubatizo mmoja "Efe.4:5 Upo mmoja tu mwingine ni wa bandia
- Je, Yesu alibatizwa namna gani?
"yesu ......akabatizwa na yohana katika yordani.mara alipopanda kutoka majini, akaona mbingu zinapasuka. " Mk.1:9,10.
- .Mtu anaweza kufanya nini Ili abatizwe?
- Kujifunza mapenzi ya Mungu. (Mt.28:19,20).
- Kuuamini ukweli wa neno La Mungu (mk. 16:16).
- 3.Kutubu na kuziacha dhambi zake na kuongoka. (mdo. 3:19).
- Ubatizo huonyesha matukio matatu ya mhimu katika maisha yako muumini wa Kweli.
- Kuifia dhambi
- Kuzaliwa upya katika Kristo na
Ahsanteni Sana kwa kusoma ujumbe huu wa Kristo na Mungu awabariki woote.Amina.
Comments
Post a Comment