Chelsea na sunderland Mmmh matatani kwa kosa La kupanga mechi Habari zaidi na karuti dickson
Chelsea wamebeba ubingwa wa mara ya 5 katika ligi kuu, hakika wiki hii ni nzuri kwao na pia kwa kocha wao Antonio Conte kwa kuwa wana jambo kubwa la kujivunia. Lakini sasa Chelsea wameingia matatani baada yakubainika kwamba mchezo wao wa mwisho dhidi ya Sunderland waliupanga kabla ya mchezo kuanza. Sheria za chama cha soka Uingereza zinasema “hairuhusiwi kupanga matokeo, au mashindano au tukio lolote katika mchezo huo kinyume na mipango ya chama cha soka” Sasa wakati wa mchezo kati ya Chelsea na Sunderland, mlinzi mkongwe wa Chelsea John Terry alitolewa uwanjani baada ya kucheza uwanjani kwa dakika 26 tu, swali likaja sub hiyo inatokeaje dakika ambayo ndio namba ya jezi ya Terry? Baada ya filimbi ya mwisho kocha wa Sunderland David Moyes alikiri kwamba kulikuwa na mpango maalum kumuaga Terry ambapo dakika ya 26 wangeufanya mpira usimame ili afanyiwe sub. Chelsea inaonekana walifanya makubaliano na Sunderland kabla ya mchezo huo ili kutekeleza jambo hilo dakika ya 26 namba am...